Kumbukukumbu ya MV Bukoba

    

Tarehe kama ya leo (Mei 21) mwaka 1996 meli ya MV Bukoba ilizama katika Ziwa Victoria. Usiku wa kuamkia siku ya ajali, meli hiyo ilipakia abiria kati ya 750 na 800 pamoja na wafanyakazi 37. Kati ya hao, 114 waliokolewa wakiwa hai; wakati 391 waliopolewa wakiwa wamefariki na kuzikwa katika makaburi ya Igoma, nje kidogo ya Jiji la Mwanza.
        Miili mingine ilichukuliwa na jamaa kuzikwa kwao. Jumla ya miili 332 haikupatikana. Kila mwaka, ifikapo Mei 21 tunawakumbuka waliopoteza maisha katika ajali hii. MV Bukoba ilijengwa na kampuni ya Kibelgiji na ilizinduliwa 27 Julai 1979. Mungu aendelee kuwalaza mahali pema peponi waliopoteza maisha na kuwafariji waliopotéza maràfiki na wanafamilia.

No comments: