Kamanda wa polisi atajwa, kifo cha kamanda Barlow, Mwanza.

Taarifa zilizozagaa hivi sasa katika mitandao zinadai kuwa
aliyekuwa kamanda wa Jeshi la Polisi mkoa wa Mwanza ameuawa na genge
ndani ya Polisi akiwemo Kamanda Polisi anayejulikana kwa jina la Muna.
       Katika tovuti ya gazeti la Jamhuri, Deo Balile anaonekana kulalamikia gazeti hilo kununuliwa kwa jumla na watu wasiojulikana.
          Kuvuja kwa siri hiyo kumetokana na mmoja wa jambazi sugu ajulikanaye kwa
jina la Edward Malele kujisalimisha ktk vyombo vya ulinzi na kutoa siri
zote.
Jambazi huyu aliombwa wa genge ndani ya polisi kushiriki katika mpango
wa kumwua kamanda Barlow. Akakataa kwa kuwa aliwahi kumfahamu kwa karibu
kamanda Barlow.
          Baada ya kukataa kutekeleza agizo hilo baada ya siku chache alishtakiwa
kwa kosa la ujambazi na kuswekwa Rumande.
Akiwa huko ndani ya wiki moja alisikia habari za kifo cha kamanda
Barlow. Akajua akina na Muna aliowakatalia wamefanya kazi aliyoikataa
yeye. Na alijua yuko mahabusu kwa sababu ya kukataa mradi huo.
Baada ya kukaa huko muda mrefu bila shitaka kueleweka wala mshataki wake
huko Lupango walimua kumwaichia. Akagoma kutoka kwa sababu anajua kuwa,
kwa kuwa amepelekwa huko ili kuficha siri hivyo, akitoka lazima
atauawa. Baada ya muda akaamua kukubali kutoka lupango na kukimbilia
kituo cha JWTZ huko Mwanza.
         Huko JWTZ Alijieleza vya kutosha na wanajeshi walimwonea huruma wakampa
Tsh 10,000/= ilie aende Bungeni huku wakiwa wamemkabidhi namba za simu
za wabunge 2 wa upinzani ili wamsaidie.
Kutokana na kutokuelewa kwake alipokuwa anashangaa shangaa katika eneo
la Bunge, alikamatwa na polisi wanalinda eneo hilo. Polisi hao wakapiga
simu Dodoma central na Mwanza. Haraka haraka mwanza wakataka arudishwe
mwanza kwa kuwa ni jambazi sugu.
          Hata hivyo, kwa katika kurupushani hiyo taarifa zimeshameshamfikia Pinda
na Nchimbi ambapo gazeti linaripoti kuwa Pinda ameagiza kijana huyo
apewe ulinzi na asirudishwe mwanza.
Tarifa zaidi zinaema kuwa mpaka sasa amepelekwa kusiko julikana.

2 comments:

Anonymous said...

hv kweli unaweza kutoka mwanza hadi dodoma kwa nauli ya shs 10,000

Justin Kasyome said...

ha haaaa! nauli ya elfu kumi kwa kuunga unga hiyo!